Free Web Hosting Provider - Web Hosting - E-commerce - High Speed Internet - Free Web Page
Search the Web

Windozi sehemu ya Tatu (windows part Three)
Matumizi muhimu yanayohusiana na windozi 95 na kuendelea
[Using Windows 95 and Later]
Mafaili na folda/Files and Folders:

Faili ni kile kinachohifadhia habari au nyaraka.

Kutafuta mafaili katika kompyuta yako (Finding Files On Your Computer):

Kama ukitaka kutafuta mafaili yako uliyoyahifadhi ndani ya kompyuta yako tumia njia zifuatazo hapo chini.
  1. bonyeza kwenye kitufe cha kuanza (Start) chini upande wa kushoto wa kioo cha kompyuta yako.
  2. bonyeza kwenye Tafuta (Find)
  3. chagua Tafuta mafaili (Find Files) au Folda (Folders)



  4. Kisha andika kwenye kiboksi jina la faili unalolitafuta. Hulazimiki kujaza kila sehemu. Muhimu ni jina la faili unalolitafuta. Kama utakuwa hujalipata na unakumbuka vitu kama tarehe sehemu pia unaweza kuvitumia
  5. Bonyeza kitufe kilichoandikwa tafuta sasa (Find Now)





Pia unawezakutafuta mafaili au faili kwa njia hizi:

Kwenye kisanduku cha kutafutia mafaili kuna sehemu iliyoandikwa "Named" hapa waweza kuandika neno lolote au jina la faili unalolitafuta na ukatafutiwa Mafano :

Katika kutafuta faili unaweza kutumia alama *. Kwa kutumia alama hii win* humaanisha kwamba mafaili yote yanayoanzia na win

Pia unaweza kutumia *.doc kumaanisha kuwa unatafuta mafaili yote yanayoishia na neno .doc

Chini ya sehemu iliyoandikwa named unafuatia mstari ulioandikwa Containing text.katika kisanduku hiki endapo utaandika neno "kompyuta" basi utatafutiwa kila faili lililo na neno "kompyuta"

Chini ya mstari ulioandikwa Containing tex kuna mstari wa mwisho ulioandikwa "Look in".

Katika kisanduku cha mstari huo panakupa uweza wa kurahisisha utafutaji wako wa mafaili kwa kugawanya utafutaji wako kwenda kwenye sehemu mbalimbali; Mafano ukichagua C: utapata mafaili yote yaliyoko kwenye hadidiski.

Pia ukichagua My document utapata mafaili na folda zote zenye muundo wa doc pekee.

Kuyatafuta au kuyaangalia mafaili ambayo uliyatumia muda mfupi uliopita

(Locating Your Most Recent Files)


  1. Kurasa za microsoft hukurahisishia wewe kupata au kuyaona mafaili hayo haraka.
  2. Bonyeza kitufe kilichoandikwa Anza kilichopo chini ya kioo cha kompyuta mkono wako wa kushoto)
  3. Bonyeza palipoandikwa nyaraka (Documents)
  4. Chagua faili unalolitaka kisha libonyeze litafunguka.



    Nyaraka za hivi karibuni(Recent Documents)

Back to top


Namna ya kukopi faili au folda kuingiza kwenye" disketi/flopi diski "A", "Desktop", "My document", "Mail recipient" au mail recipient kupitia "Microsoft Outlook".

  1. Chagua fold au faili unalotaka kulikopi/kuhamisha
  2. Bonyeza kiongozeo/mausi yako kwenye kitufe cha upande wa kulia.
  3. Chagua neno peleka/hamishia (send to..).
  4. chagua 3.5 Flopi/Floppy "A"



    hamishia/peleka
  5. Unaweza pia kuliburuza hilo faili kwenda kwenye 3.5" Flopi/Floppy (A:\) upande wa kushoto.

kuhamisha au kukopi faili/folda kutoka flopi/floppy diski/disk kwenda kwenye draivu nyingine.

  1. Chagua 3.5 Flopi/Floppy (A:) upande wa kushoto
  2. chagua faili/folda unalotaka kulikopi toka kwenye flopi diski kwenda kwenye draivu unayotaka kuhamishia/kukopia.
  3. Pia unaweza kuliburuza kwa kutumia mausi/kiongozeo bila kuikiachia hadi kwenye draivu aunayotaka kuhamishia/kukopia.




Unaweza kufungua windo mbili kama hapo pichani na zisogeze hadi ziweze kuonekana katika windo moja na kisha katika windo hizo moja ukachagua sehemu unakotaka faili lihamishiwe baada ya kuliburuza na ile windo ya pili ukachagua huko lile faili unalolitaka lihamishwe.

Katika kukopi kwa kuburuza hapa unaweza kukopi na kubakisha nakala/kopi kwa kushikilia kitufe cha -Ctrl- wakati wa kuliburuza

Pia unaweza kukopi na kulihamisha faili bila kuacha nakala/kopi kwa kushikilia kitufe cha -shift- wakati unapokuwa unaliburuza

Kukopi na kuacha nakala/kopi unatakiwa ukliki faili unalotaka halafu unashikilia kitufe cha control-Ctrl- na kisha unaliburuza faili hadi pale unapopataka na kisha liachie.

Kukopi bila kuacha nakala/kopi kliki faili unalotaka kulihamisha na kisha shikilia kitufe cha -Shift- halafu liburuze hilo faili hadi pale unapopataka kuliweka na kisha liachie

Pia unaweza kulikliraitikliki faili;
Kisha ukalikopi au kukati [copy/cut and paste],



Halafu ukafungua sehemu mpya unakotaka kuliweka,
Ukapakliki na kisha ukalipesti lile faili.




Kubadilisha faili/folda jina (Renaming A File or Folder)

  1. Chagua faili au folda unayotaka kuibadilisha jina.
  2. Libonyeze upande wa kulia
  3. Chagua neno badili jina (Rename)
  4. Halafu badili jina.

    kubadili faili/folda jina

    kubadili faili/folda jina



[
Back to top] [Rudi nyuma (Back)-Windows2]
[ Rudi Kwenye yaliyomo-Contents][Endelea(Next)-Mdahalishi]